Monday, November 4, 2013

 
SIKU chache baada ya serikali kusitisha Opereshini Tokomeza Ujangili kutokana na wabunge kuilalamikia wakidai inakiuka haki za binadamu na mifugo mingi imeuawa, siri imefichuka kwamba baadhi ya wabunge na vingozi wa serikali wanatumiwa na majangili kudhoofisha vita dhidi ya ujangili.
Kwa mujibu wa vyanzo vyetu kutoka bungeni na serikalini, majangili hao wamegawanyika katika makundi sita. Wamo wafugaji, wakulima, watalii, wamiliki wa vitalu vya uwindaji, wabunge, na viongozi wa serikali ambao wameibuka na kuingilia kati baada ya kuhisi kwamba wanakaribia kukamatwa.
Tanzania Daima limedokezwa kuwa zaidi ya sh milioni 200 zimechangwa na majangili hao kwa ajili ya kufanikisha mkakati wa kuzima opereshini hiyo.
Baadhi ya wabunge wanatumiwa bila kujua, huku wengine wakifanya hivyo kwa hiari na makusudi ya kunusuru majangili.
Tayari kuna mpasuko mkubwa serikalini na ndani ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) kutokana na baadhi ya watendaji kubaini mbinu chafu za kutaka kuzima operesheni hiyo ili kuwanufaisha vinara wa ujangili.
“Hawa watu wana mtandao mkubwa, baada ya kubaini wanakaribia kunaswa, sasa wameingia bungeni kwa kuwatumia baadhi ya wabunge ili waipinge operesheni hiyo,” kilisema chanzo.
Taarifa za uhakika kutoka serikalini zinasema kuwa majangili hao wamekuwa na jeuri kutokana na kuwazunguka viongozi wa chini na kuwasiliana moja kwa moja na kigogo, ambaye bila kujua amekuwa akizunguka viongozi wa wizara, na kukingia kifua majangili.
Baadhi ya vyanzo hivyo vilieleza kushangazwa na hatua ya baadhi ya wabunge kutetea uhai wa ng’ombe na kushindwa kulinda uhai wa tembo wanaouawa na kung’olewa pembe.
Mwishoni mwa wiki, Bunge liliazimia kuunda kamati teule ili kuchunguza suala hilo huku Waziri Mkuu na mawaziri wanne wakisulubiwa kwa madai kuwa  wameshindwa kuwajibika ipasavyo.
Mbali na Pinda, wamo pia Dk. Emmanuel Nchimbi (Mambo ya Ndani), Khamis Kagasheki (Maliasili na Utalii), David Mathayo David (Mifugo na Uvuvi) na Shamsi Vuai Nahodha (Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa).
Hata hivyo, gazeti hili limedokezwa kuwa kwa vyovyote iwavyo serikali haitakuwa tayari kukubali kamati teule hiyo iundwe kwani ripoti yake inaweza kumng’oa Pinda na hivyo serikali kuanguka.
“Kinachofanyika sasa ni kuletwa kwa taarifa ya dharura bungeni ya kuonyesha serikali inapendekeza njia mbadala ya kushughulikia suala hilo ili badala ya kamati teule, iundwe tume huru itakayoongozwa na jaji kama ambayo CHADEMA wamekuwa wakipendekeza muda mrefu.
“Vita hii ya ujangili ni pana, imeingia hadi kwenye siasa za makundi ya urais ndani ya CCM, na hivyo kundi moja linataka kumng’oa Makinda kwenye uspika kwa hofu kuwa anawasikiliza sana wabunge na mawaziri wa kundi jingine,” kilisema chanzo hicho.
 
Kwamba Oparesheni Tokomeza Ujangili inapingwa baada ya vinara hao kubaini wanakaribia kunaswa, na sasa wanataka kuvuruga ili kazi hiyo irudi nyuma na hata ikiendelea basi wako radhi kutajana kwa majina kwani miongoni mwao wamo pia wabunge na viongozi wengine.
“Hawa majangili wana jeuri, wao wanazungumza kwa simu moja kwa moja na mmoja wa vigogo wa ngazi za juu serikalini, na huko wanasikilizwa. Serikali nayo inajua kuwa operesheni ikisimama tembo wanakwisha na vile vile kamati teule wakiikubali serikali inaanguka,” kinasisitiza chanzo.
Vyanzo hivyo vinaainisha kuwa hata mchakato wa kutaka kumwondoa Makinda kwenye uspika ambao ulikuwa umeanza kupitia kwa Mbunge wa Nzega, Dk. Hamis Kigwangalla kukusanya kura za wabunge uliingiliwa na majangili hao.
Vyanzo vya habari vinasema hoja ya Kigwangalla inasukumwa na wakubwa kadhaa mashabiki wa mmoja wa mawaziri waandamizi wanaotajwa kutaka kugombea urais 2015, ambao wanaona Makinda anapendelea wabunge wanaoshabikia kambi ya kigogo mwingine anayesemekana kutaka urais kwa udi na uvumba.
Habari zinasema kundi la waziri huyo linaungwa mkono na kigogo mmoja mwandamizi ambaye hataki kabisa kuruhusu swahiba wake wa zamani agombee urais; na sasa wamedhamiria kumwangusha Makinda.
Hata hivyo, kabla hoja yao haijashika kasi, wakati wakiendelea kukusanya sahihi za kutosha kumwondoa Makinda, majangili nao wakapata upenyo kwa kuathiri mwelekeo wa Bunge, na Makinda anaruhusu mjadala wa ujangili, ambao iwapo kamati teule itaundwa na kufanya kazi yake barabara, serikali inaweza kuangushwa kabla ya spika huyo kuondolewa.
“Hoja ya Makinda imezimwa, sasa wabunge wanazungumzia operesheni ya ujangili. Hapa wanajua kuwa spika hawezi kukubali hoja hiyo iendelee, hivyo naye ataipa kipaumbele kamati teule ili kuonyesha serikalini kuna tatizo.
“Wanajua hawawezi kumfukuza spika katika kikao hiki, lakini wakati huo Kamati ya Bunge itakuwa imekamilisha mchakato na kutoa uamuzi dhidi ya Pinda na mawaziri wenzake, jambo ambalo linaweza kumnusuru Makinda na kuiangusha serikali,” kilisema chanzo chetu.
Mbunge wa Sikonge, Said Nkumba (CCM), ndiye alitaka Bunge lijadili kuhusu migogoro kati ya wafugaji na watumiaji wengine wa ardhi, huku Mbunge wa Mwibara, Kangi Lugola (CCM), akitaka Bunge lijadili vitendo vinavyofanywa na watendaji katika Operesheni Tokomeza Ujangili.
Lugola alidai watendaji wamekuwa wakiwaua kwa risasi ng’ombe waliowakamata kwenye operesheni hiyo pamoja na kuwatesa wamiliki wasiotoa fedha zinazohitajika.
Kutokana na hoja hizo, Makinda alitoa fursa kwa Waziri wa Maliasili na Utalii, Kagasheki na Waziri wa Maendeleo ya Mifugo na Uvuvi, Mathayo, kuelezea Operesheni Tokomeza Ujangili na migogoro kati ya wafugaji na watumiaji wengine wa ardhi. 
Kagasheki ndiye aliyekuwa wa kwanza kueleza operesheni hiyo inaendelea. Alisema inalenga kutokomeza ujangili ulioshamiri hapa nchini kiasi cha kutishia sekta ya utalii na tembo.
Hata hivyo, Kagasheki alisema kutokana na malalamiko ya watu mbalimbali juu ya mwenendo wa operesheni hiyo, serikali imeamua kuisitisha ili kufanya tathmini.
Waziri huyo pia alisema mifugo yote iliyokamatwa ndani ya hifadhi kabla na baada ya operesheni hiyo iachiliwe bila gharama yoyote na watu wenye ushahidi wa ng’ombe wao waliouawa kwa risasi wawasilishe vielelezo ili achukue hatua zaidi.
Waziri Mathayo alitoa taarifa kuhusu migogoro kati ya wafugaji na wakulima. Aliwaomba radhi waliopata hasara ya kujeruhiwa, kupoteza mifugo au vifo katika operesheni hiyo.

0 comments:

 

Tuesday, August 13, 2013


Home
Habari
Kamati ya Bunge yakwama kukagua hesabu Mwanza
Mwanza
Toleo la 310
7 Aug 2013
UHAMISHO uliofanywa na Ofisi ya Waziri Mkuu, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) kwa mkurugenzi na baadhi ya wakuu wa idara katika Halmashauri ya Jiji la Mwanza mapema mwaka huu, umekwamisha Kamati ya Bunge ya Hesabu za Serikali za Mitaa (LAAC), kukagua hesabu za halmashauri hiyo.
Taarifa zilizolifikia gazeti hili zinaeleza kuwa kamati hiyo ilishindwa kukagua hesabu za halmashauri hiyo kwa kuwa watendaji wengi ambao wangetakiwa kujibu hoja mbalimbali za kamati hiyo ni wageni na hivyo kwa mazingira hayo, hakuna tija ya kufanya ukaguzi huo.
Makamu Mwenyekiti wa kamati hiyo, Suleiman Zedi, ameliambia Raia Mwema kuwa kamati yake imeshindwa kutimiza wajibu wake kwa kuwa si rahisi kuhoji watendaji ambao ni wageni katika halmashauri hiyo.
"Mahesabu (hesabu) tunayokagua yanaishia Juni mwaka huu, mkurugenzi aliyepo ninaambiwa ana miezi miwili, wale wote waliongia mikataba na kulipa wakandarasi hawapo, kama kuna matatizo na hoja za kujibu huyu hana majibu," alidai Zedi, ambaye ni Mbunge wa Jimbo la Bukene, mkoani Tabora, kupitia Chama cha Mapinduzi (CCM).
Kamati hiyo imeagiza TAMISEMI kuwarejesha watumishi wote baadaye mwezi huu ili kujibu hoja za kamati za kamati hiyo na zile zilizoibuliwa katika ripoti ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) kwa halmashauri hiyo.
Watumishi hao wanaotakiwa kurejea ili kujibu hoja za kamati hiyo ni pamoja na aliyekuwa Mkurugenzi wa Jiji la Mwanza ambaye kwa sasa ni Murugenzi wa Jiji la Dar es Salaam, Wilson Kabwe, aliyekuwa mweka hazina ambaye sasa ni Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Njombe, William Ntinika, aliyekuwa mchumi wa Jiji ambaye sasa ni Mkurugenzi  wa Halmashauri ya Wilaya ya Msalala mkoani Shinyanga Patrick Kulangwa na aliyekuwa mhandisi wa halmashauri hiyo ambaye sasa ni Mkurugenzi Halmashauri ya Kigoma Ujiji, Boniface Nyambele.
Pamoja na uhamisho huo kikwazo kingine kilichofanya kamati hiyo kushindwa kukagua hesabu za halmashauri hiyo ni pamoja na kucheleweshwa kwa vitabu vya hesabu (kufika) ofisini kwa CAG kama inavyotakiwa na waraka wa TAMISEMI namba 2/CA.26/215.
Waraka huo unataka halmashauri nchini kuwasilisha vitabu vyao vya hesabu kwa CAG mwezi mmoja kabla ya ukaguzi kufanyika, lakini halmashauri ya Jiji la Mwanza imewasilisha ripoti hizo siku chache zilizopita na kuifanya kamati hiyo kushindwa kupata muda wa kukagua.
"Lakini pia walichelewesha vitabu vya mahesabu (sahihi hesabu) kwa hiyo hatukupata muda wa kukagua, tumeshindwa kukagua hesabu zao," alisema Zedi.
Taarifa kutoka ndani ya Jiji la Mwanza zinaeleza kuwa moja ya mambo ambayo yanaweza kuwaweka matatani watendaji hao ni pamoja na mkataba walioingia na Mfuko Taifa wa Hifadhi ya Jamii (NSSF) wa kununua viwanja katika eneo la Bugarika ambavyo walishindwa kuukabidhi mfuko huo kwa wakati.
NSSF iliingia mkataba na Halmashauri ya Jiji la Mwanza kununua jumla ya viwanja 692 kwa ajili ya kuwekeza katika ujenzi wa nyumba za kuuza kwa wanachama wao na wananchi kwa ujumla. Katika mkataba huo uliotiwa saini Agosti 18, 2008 kati ya Mkurugenzi wa Jiji la Mwanza Wilson Kabwe na Mkurugenzi wa NSSF, Dk. Ramadhani Dau ulieleza kuwa viwanja hivyo vitalipiwa jumla ya  shilingi bilioni 1.8 ( 1,887,081,700 ) kwenye maeneo ya Bugarika na Kiseke.
Hadi Januari, mwaka huu wakati Kamati ya Bunge ya Huduma za Jamii ilipofanya ziara katika Halmashauri ya Jiji la Mwanza, mgogoro huo ulikuwa ukifukuta, pamoja na NSSF kuwa ilikwisha kulipa asilimia 80 ya fedha yote inayotakiwa kulipwa bado mfuko huo ulikuwa haujakabidhiwa viwanja 267 vilivyoko Bugarika ambavyo thamani yake halisi ni shilingi milioni 812.
Mkurugenzi wa  uwekezaji wa NSSF, Yacoub Kidula alisema wakati huo kuwa kama fedha hizo (Sh milioni 812) zingewekezwa mahali pengine au katika dhamana za serikali kwa muda huo, NSSF ingepata faida kati ya asilimia 12- 13 ambayo ni sawa na shilingi milioni 105.
Kamati hiyo iliyokuwa ikiongozwa na Makamu Mwenyekiti wake (kwa wakati huo) Juma Nkamia, iliagiza Mkurugenzi wa Jiji akutane na kamati hiyo mbele ya Waziri wa TAMISEMI katika kikao cha Bunge cha Februari, mwaka huu, ili kueleza kwa nini hawajatoa viwanja kwa  NSSF, baada ya mfuko huo kukataa kupewa viwanja mbadala katika eneo la Kishiri lililopo Igoma nje kidogo ya Jiji, lililopendekzwa na halmashauri kuwa halilingani thamani na eneo walilochagua awali (Bugarika) ambalo liko jirani na Hospitali ya Rufaa ya Bugando na Chuo Kikuu cha Sayansi ya Tiba cha Bugabdo (CUHAS)
Hoja nyingine ambazo ziliibuliwa na ripoti ya CAG kwa mwaka wa fedha 2011/2012 ni  pamoja na kutotekeleza mapendekezo ya ukaguzi ya miaka iliyopita ambayo yalifikia shilingi billioni 1.7 na kutozingatia viwango vya kimataifa vya uaandaaji wa taarifa za fedha kwa sekta ya umma (IPSAS).
Kwa mujibu wa IPSAS, mali zinazooneshwa kwenye taarifa ya hesabu zinazotolewa zithaminiwe na kutambuliwa na kwamba zitaendelea kutambuliwa katika hesabu kwa kiasi ambacho kimethaminishwa. Thamani inayotambuliwa itazingatia kutolewa kwa thamani ya uchakavu na hasara inayotokana na ujumla wa kuharibika kwa mali.
Kinyume na mwongozo huu, uongozi wa halmshauri ya jiji umeingia katika kundi la halmashauri 13 ambazo hazikuthaminisha mali zake ingawa baadhi ya mali hizo zilioneshwa katika hesabu kama ni mali ambazo hazina thamani kabisa wakati katika hali halisi mali hizo ziliendelea kutumiwa na halmashauri.
Kutokana na hali hii, thamani ya mali za kudumu zilizooneshwa katika taarifa za fedha za halmashauri hazitoi taswira halisi ya halmashauri. Kwa mujibu wa ripoti hiyo ya CAG Jiji la Mwanza lilikuwa na vifaa 37 ambavyo havijathaminishwa.
Hoja nyingine zilizoibuliwa na ripoti ya CAG ya mwaka 2011/2012 ni pamoja na matumizi ya vifungu visivyohusika yaliyofikia shilingi milioni 22.5 na watumishi 100 waliokopa zaidi ya kiwango kinachotakiwa.
Mkurugenzi wa halmashauri hiyo, Halifa Hida, alipotafutwa kueleza kwa nini walichelewesha taarifa za hesabu zao kwa CAG kinyume na waraka unavyotaka, alijibu yuko safarini na kushauri atafutwe kaimu wake ambaye ndiye aliyekutana na kamati hiyo.
Hata hivyo, Kaimu Mkurugenzi huyo Francis Mkabenga alipotafutwa na mwandishi wetu alijibu ya kuwa ana mambo mengi ya muhimu ya kufanya kuliko hilo.
"Sisi tumewaeleza kamati wameelewa na ndiyo maana wametupa wiki mbili, sasa hivi ninafanya mambo ya maana zaidi kuliko hilo siwezi kuwa naeleza kila mtu, nilieleza kwenye kamati waulize wao (kamati)," alijibu Kaimu Mkurugenzi huyo.
Soma zaidi kuhusu:
Tufuatilie mtandaoni:
Endelea Kuhabarika
Toa maoni yako
Top of Form
Your name
E-mail
The content of this field is kept private and will not be shown publicly.
Homepage
Comment *
Text format
  • Web page addresses and e-mail addresses turn into links automatically.
  • Allowed HTML tags: <a> <em> <strong> <cite> <blockquote> <code> <ul> <ol> <li> <dl> <dt> <dd>
  • Lines and paragraphs break automatically.
Image CAPTCHA
What code is in the image? *
Enter the characters shown in the image.
Bottom of Form
Top of Form
Search form
Search
Bottom of Form
Maoni ya Wasomaji
·       brother,suala la madawa ya kulevya hapa tanzania halina mwenyewe,je unajua kuwa dogo r naye alinaswa na mdude kule china?kak jk akawa mpole ,na bosi wa china akatua kuchukua tenda mbalimbali za mak
11 hours 37 min
Yametolewa maoni mengine 2
Makala Pendwa
Mwandishi Wetu
32,102
Waandishi Wetu
29,782
Mwandishi Wetu
27,449
Waandishi Wetu
23,736
Mwandishi Wetu
22,532
Kura ya Maoni
Kwa wale wenye vitambulisho vya kupiga kura, je uchaguzi wa 2010 ulipiga kura?
Ndiyo
60%
Hapana
40%
Total votes: 948
·       Yaliyopita
Tunapatikana Facebook
Lango la Wenyeji
Top of Form
Jina *
Siri *
·       Jisajili
·       Badilisha siri
Bottom of Form
Wasome zaidi Waandishi wa Raia Mwema
Copyright © 2013 Raia Mwema Newspaper Company unless otherwise noted. All rights reserved.
http://www.raiamwema.co.tz/sites/all/themes/mayo/images/up-arrow.png
Habari
Akaunti ya kigogo TANESCO yazuiwa
Waandishi Wetu
Toleo la 250
18 Jul 2012
Mkurugenzi Mtendaji wa TANESCO, William Mhando
  • Yakutwa na zaidi ya Sh. bilioni moja, uchunguzi waendelea
  • Mpango wa kupandikiza mgawo ‘feki’ wa umeme wafichuliwa
SIKU chache baada ya kusimamishwa kazi kwa Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Umeme (TANESCO), William Mhando na wenzake: Robert Shemhilu, Lusekelo Kassanga na Haruna Mattambo, akaunti ya mmoja wa vigogo wa shirika hilo ngazi ya menejimenti iliyoko katika moja ya benki nchini imezuiwa na vyombo vya dola nchini, Raia Mwema, limeelezwa.
Akaunti ya kigogo huyo (jina la benki na la mwenye akaunti yanahifadhiwa ili kutoharibu uchunguzi unaoendelea) imekutwa na fedha zaidi ya shilingi bilioni moja na sasa inadaiwa kuzuiwa kwa baraka za mamlaka za juu.
Vyanzo kadhaa vya habari vimeeleza ya kuwa kigogo huyo amekutwa na mabilioni hayo ya fedha huku chanzo cha mapato hayo yasiyolingana na kipato chake kama mtumishi wa umma kikiwa ni utata.
Hata hivyo, wakati uchunguzi huo wa awali unaofanywa na vyombo vya dola nchini ukiwa unaendelea, kwa upande mwingine kumebainika kuwapo na kampeni kali za kuuokoa uongozi wa TANESCO unaochunguzwa kwa sasa, juhudi ambazo zimekuwa zikihusisha hata Kamati za Bunge.
Kamati za Bunge ambazo baadhi ya wajumbe wake wanahusishwa katika ‘kuokoa’ jahazi la uongozi wa TANESCO uliosimamishwa ni pamoja na Kamati ya Bunge ya Nishati na Madini na Kamati ya Bunge ya Hesabu za Mashirika ya Umma.
Baadhi ya wajumbe wa kamati hiyo sasa wanatajwa kuanza kumwandama Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati na Madini, Eliakim Maswi pamoja na Waziri Profesa Sospeter Muhongo na Naibu wake, George Simbachawene, wanaotajwa kuwa na msimamo mkali dhidi ya kile kinachodaiwa kuwa ni uzembe na ubadhirifu ndani ya TANESCO.
Mgawo feki wa umeme
Kwa mujibu wa taarifa zilizopo, kwa muda mrefu sasa kumekuwa na njama za kuandaa na kufanikisha mgawo ‘feki’ wa umeme nchini kwa njia mbalimbali. Lengo la mgawo huo ni kuwanufaisha baadhi ya vigogo TANESCO kwa njia ya ununuzi wa mafuta ya kuendeshea mitambo.
Uchunguzi uliofanywa na gazeti hili na kuthibitishwa na vyanzo mbalimbali vya habari ndani ya Wizara ya Nishati na Madini pamoja na TANESCO, umebaini kuwa baadhi ya mitambo ya kuzalisha umeme jijini Dar es Salaam, na hasa baadhi ya mitambo iliyopo eneo la Ubungo na Tegeta imekuwa ikizimwa ili kuhalalisha migao na mpango wa ununuzi mafuta unaowaingizia fedha vigogo. Orodha ya mitambo inayozalisha umeme kwa mafuta jijini Dar es Salaam ni pamoja na IPTL, Symbion na Aggreko.
Taarifa zilizopo zinazidi kubainisha kuwa, baada ya kuzima mitambo hiyo na kusababisha mgawo wa umeme (usio wa lazima-feki), wito wa kuzalisha umeme wa mafuta hujitokeza.
Ni katika wito huo ambao msingi wake ni kupandikiza mgawo feki wa umeme, wakati mwingine Serikali hutoa fedha za ununuzi wa mafuta lakini wakati mwingine fedha hizo huchotwa kutoka TANESCO, shirika ambalo kila mwezi hukusanya shilingi karibu ya bilioni 100 kutoka kwa wateja wake.
Katika ununuzi huo wa mafuta kwa ajili ya kuendesha mitambo ili kuongeza uzalishaji wa umeme, mambo kadhaa huzingatiwa ili kunufaisha wahusika.
Jambo la kwanza ni kupatikana kwa kile kinachoitwa “ten percent” kinachogawanywa kwa waliofanikisha mpango huo. Pili, ni kuendelea kufanya wizi katika kiwango cha mafuta kilichokwishakununuliwa kwa ajili ya kuwasha mitambo husika.
Mchezo huo mchafu unadaiwa kuripotiwa kwa baadhi ya viongozi wa TANESCO lakini hapakuwa na hatua zilizopata kuchukuliwa hadi pale suala hilo lilipofika katika uongozi wa Wizara ya Nishati na Madini.
“Suala hili limekuwa likifanyika kwa muda mrefu sasa, umeme unakatwa na kuzalishwa kwa kiwango cha chini ili kuibua mahitaji ya kuzalisha umeme kwa njia ya mafuta ili TANESCO wanunue. Katika ununuzi huo kuna suala la 10% na wizi wa hayo hayo mafuta yanayonunuliwa lakini pia ni manufaa kwa kampuni za uzalishaji umeme huo kwa kuwa zinakuwa zikifanya biashara kwa kuuza umeme huo TANESCO.
“Ni suala lililowahi kuripotiwa lakini likapuuzwa na menejimenti, ila miezi takriban mitatu kupita baada ya kuripotiwa kuliwahi kufanyika kikao cha wafanyakazi wote kupitia TUICO, baada ya wafanyakazi kutia shinikizo kuhusu hujuma hizi Mkurugenzi wa TANESCO, Mhando naye ndipo akadai kupata taarifa hizo hapo kwa mara ya kwanza na aliahidi kuchukua hatua,” kilieleza chanzo kimoja cha habari.
Hujuma kwa mtambo wa Kinyerezi
Hujuma nyingine inayotajwa kufanyika ndani ya TANESCO ni kuahirishwa mara kwa mara kwa mchakato wa kuanzisha mtambo wa kuzalisha umeme eneo la Kinyerezi, jijini Dar es Salaam.
Mtambo huo ambao utazalisha umeme kwa kutumia gesi, unatajwa kuwa tishio dhidi ya mtandao wa wauzaji mafuta kwa TANESCO kwa ajili ya uzalishaji umeme kwa kutumia mafuta.
“Kutokana na tishio la mradi huu utakapokamilika kuwanyima ulaji, walikuwa wakiukwamisha. Ni mradi wa megawati 240. Huu (mradi wa Kinyerezi) utaua kabisa mpango wao wa ulaji kwa kuandaa mgawo feki na kuzalisha umeme kwa mafuta. Waziri Muhongo alipoingia alihakikisha mradi unasainiwa ili kuanza....lazima wampige vita na aliwaeleza katika moja ya vikao (waziri) kuchukizwa na tabia hiyo,”
Wabunge nao watajwa
Mbunge mmoja wa Viti Maalumu kutoka mikoani (kwa sasa hatutamtaja kwa kuwa hatukufanikiwa kumpata) anadaiwa kunufaika na uongozi wa TANESCO uliosimamishwa.
Kwa mujibu wa taarifa zilizotufikia,mbunge huyo anadaiwa kupewa zabuni ya kusambaza matairi kwa ajili ya magari ya TANESCO kupitia kampuni yake. Madai yanayoelekezwa kwa mbunge huyo ni kwamba, kampuni yake ilipewa zabuni baada ya zabuni hiyo ‘kuporwa’ kutoka kwa kampuni nyingine.
Lakini wakati mbunge huyo wa Viti Maalumu  akihusishwa na madai hayo, mbunge mwingine na Kiongozi wa Kambi ya Upinzani, Freeman Mbowe, naye anadaiwa kuwa na maslahi na uongozi uliosimamishwa wa TANESCO.
Kwa mujibu wa vyanzo kadhaa vya habari, Mbowe, ambaye ni Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA)  amekuwa katika mazungumzo yanayotajwa kwenda vizuri ili auziwe mtambo wa kufua umeme unaoitwa Kikuletwa, ulioko katika Jimbo la Hai, ili baada ya kununua aweze tena baadaye kuiuzia umeme TANESCO kama inavyofanyika kwa kampuni nyingine za uwekezaji nchini ambazo kwa muda sasa zimekuwa zikitajwa kuuza umeme kwa bei kubwa.
Raia Mwema halikufanikiwa kumpata Mbowe kusikia maelezo yake, lakini mmoja wa viongozi wa kurugezi za chama hicho, John Mrema, amemweleza mwandishi wetu kuwa anayetaka kununua mtambo huo si Mbowe binafsi bali ni Halmashauri ya Wilaya ya Hai.
“Mbowe kama mbunge alikuwa akisaidia kufanikisha hilo. Mpango uliopo ni kununua mtambo huo wa siku nyingi ambao hautumiki ni kuukarabati na kisha kuanza kuzalisha umeme ambao sehemu itatumiwa na wananchi wa Hai na kiasi kingine cha umeme kitauzwa TANESCO,” alisema Mrema.
Suala la kusimamishwa kwa uongozi huo wa juu wa TANESCO limevuta hisia nyingi huku makundi ya watu wakipita huku na kule kujaribu kubatilisha uamuzi huo, mengine yakidai kwamba taratibu za kuusimamisha zimekiukwa, mengine yakivurumisha tuhuma nzito dhidi ya uongozi wa wizara na mengine yakitaka Bodi nzima ya TANESCO iondolewe kwa vile baadhi ya wajumbe wa Bodi hiyo wamekuwa wakifanya biashara ya mafuta na shirika hilo.
Raia Mwema limefahamishwa kwamba timu ya uongozi wa wizara jana ilikuwa Dodoma ambako iliitwa kwenda kujieleza mbele ya Kamati za Bunge zinazohusiana na TANESCO.
Tarifa zaidi zilizopatikana tukienda mitamboni zilieleza kwamba pamoja na kukutana na kamati hizo, timu hiyo ya wizara imeomba kukutana kwanza na kamati ya CCM ambako mtoa habari wetu ametufahamisha kwamba patamwagwa kila kitu hadharani kuhusiana na nani wanahujumu TANESCO, nani wanaofadika nayo na kwa njia zipi.
Kusimamishwa kwa Injinia Mhando na wenzake kulikuja kiasi cha siku tatu tu baada ya Raia Mwema kuripoti taarifa za kuwako makundi ya wafanyakazi wa Wizara ya Nishati na Madini na wenzao ndani ya mashirika na taasisi tanzu za wizara hiyo, wanaohujumu jitihada za sasa za kuisuka upya wizara na taasisi na mashirika yake.
Jitihada hizo, kwa mujibu wa vyanzo mbalimbali vya habari serikalini, zimekuwa pia zikiwahusisha kwa karibu baadhi ya wenyeviti wa bodi za mashirika na taasisi hizo na watendaji wakuu wake ambao wanahisi ya kuwa, kwa mazingira mapya wizarani, ajira zao zinakaribia ukingoni kutokana na ama utendaji binafsi usiokidhi au kwa kushindwa kudhibiti uozo katika taasisi na mashirika yao.   
Kwa mujibu wa taarifa hizo, mtandao wa makundi hayo ulioungana ulikuwa ukiendesha kampeni ya kuukataa uongozi wa wizara kwa madai kwamba umekuwa ukiendesha mambo kibabe.
Raia Mwema limedokezwa pia kwamba nje ya wizara, taasisi na mashirika yake, mtandao huo unaungwa mkono na baadhi ya wabunge, wengine wakiwa katika kamati zinazohusiana na wizara hiyo, na kwamba mipango iliyokuwa inasukwa ili kupeleka ujumbe kwa mamlaka husika kuwa uongozi wa wizara haufai, uondolewe, ni pamoja na kukwamisha bajeti ya wizara itakayowasilishwa bungeni wiki ijayo.
Hoja nyingine zanazodaiwa kushadidiwa na mtandao huo kama sababu za ziada kutaka mabadiliko ya uongozi wizarani ni kuwa Waziri mpya, Profesa Sospeter Muhongo, si mwanasiasa, ubunge wake uliompa uwaziri umetokana na yeye kuteuliwa na hilo linawakera baadhi ya wabunge wa majimbo ambao wanaona si vyema wao kuachwa, mtu wa “kuja” akapewa nafasi hiyo kubwa tena katika wizara inayotajwa kuwa tajiri na yenye ulaji kama ya Nishati na Madini.
Ukiacha hilo, Raia Mwema limeambiwa pia ya kuwa  madai mengine ni suala ambalo chimbuko lake ni ukabila. Waziri Profesa Muhongo anatoka Mkoa wa Mara ambako ndiko anakotoka pia Katibu Mkuu, Eliachim Maswi, ingawa inafahamika kwamba wanatoka katika maeneo mawili tofauti ya mkoa huo. Kwa mujibu wa madai ya wana mtandao huo, Profesa Muhongo na Maswi kwa kutoka katika Mkoa mmoja na sasa wanafanya kazi ofisi moja ni tatizo.
Alipoulizwa na Raia Mwema juu ya madai hayo, mwanzoni mwa wiki iliyopita, Maswi  alisema hakuwa na namna ya kuzuia watu wasizungumze wanayoyataka. Alisema yawepo au yasiwepo, yeye na timu wanayoijenga wizarani wameamua kufanya kazi ili kuleta tija katika maeneo waliyokabidhiwa kuyasimamia.
“Rais Jakaya Kikwete aliyetuteua hakufanya hivyo ili tuje hapa tuchezecheze. Tumepewa majukumu ya kutekeleza. Hebu niambie, nyumbani kwako siku hizi umeme unakatika mara ngapi?
“Ukiona kuna mawazo kama hayo, ujue tunafanya kazi. Sisi hatutajali yanayosemwa, kipimo chetu ni kama umma unaridhika. Kama unaona baadhi ya kero zilizokuwapo, zilizokuwa ndani ya uwezo wetu, sasa zimepungua kwenye vitu kama umeme, na kama tumeanza kupata stahili yetu kwenye maeneo kama ya migodi ujue wizarani sasa kuna wachapakazi,” alisema Maswi.
Katibu Mkuu Maswi aliteuliwa na Rais Kikwete kuwa Kaimu Katibu Mkuu katikati ya Julai mwaka jana, kiasi cha mwaka mmoja uliopita, akichukua nafasi iliyokuwa imeachwa na David Jairo aliyekuwa ametuhumiwa na Bunge, pamoja na mambo mengine, kwa ubadhirifu.
Aidha, Profesa Muhongo, mmoja wa Watanzania wachache wataalamu wa jiolojia,  amejiunga serikalini mwanzoni mwa Mei, mwaka huu, baada ya kuteuliwa na Rais Kikwete kwanza kama mbunge kupitia nafasi 10 za Rais kuteua wabunge kwa mujibu wa Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
Mashirika yaliyo chini ya Wizara ya Nishati na Madini ni Shirika la Umeme (TANESCO) ambalo Mwenyekiti wake wa Bodi ni Jenerali mstaafu na mkuu wa zamani wa Majeshi, Robert Mboma, Mtendaji wake Mkuu ni Mhandisi Godfrey Mhando.
Mengine ni EWURA ambalo Mwenyekiti wake wa Bodi ni Simon Sayore; huku Mtendaji Mkuu akiwa Haruna Masebu; Wakala wa Umeme Vijijini (REA) ambalo Mwenyekiti wake wa Bodi ni Balozi Ami Mpungwe na Mtendaji Mkuu ni Dk.  Dk Lutengano Mwakahesya; Wakala wa Madini (TMAA)  ambalo Mwenyekiti wake wa Bodi ni Dk. Yamungu Kayandabila, Mtendaji Mkuu akiwa Mhandisi Paul Masanja.
Mengine ni  STAMICO ambalo Mwenyekiti wa Bodi ni Ramadhani Omari Hatibu, Mtendaji Mkuu akiwa Grey Mwakalukwa; GST lililo chini ya Uenyekiti wa Bodi wa Profesa Idrissa Kikula na Mendaji Mkuu akiwa Profesa Abdul Mruma  na TPDC ambalo Mwenyekiti wake ni Michael Mwanda na Mtendaji Mkuu  ni Yona Kilagane.

Soma zaidi kuhusu:

Tufuatilie mtandaoni:

Maoni ya Wasomaji

huyo kigogo waliyemfungia akaunti yake wanamuonea tu. mbona yule waziri anayesubiri kuota ndoto anajenga hoteli ya mabilioni kule mtwara? mbona yeye hanyanganywi?? halafu kuna waziri kijana ndani ya miaka 3 alijipatia magorofa na majumba ya bei mbaya. kwanini yeye ilionekana ni kitu cha kawaida??

Ndg. Kinyonga.
tatizo linapotokea kinachohitajika ni hatua za kulishughulikia. huwezi kusema uliache kama lilivyo eti kwasababu kuna matatizo mengine kama hayo sehemu nyingine. vinginevyo hiyo "wamemuonea" maana yake nini?. aachwe eti kwasababu kuna wengine?. ulipaswa kushauri na hao wengine washughulikiwe hivyohivyo na sio kutangaza "wamemuonea" mtu ambaye anatuhumiwa kuihujumu nchi. hiyo ina maana unaunga mkono vitendo vya kifisadi. acha ndg. yangu namna hiyo sio uungwana.!

sisi watanzania watu wa ajabu sana, kila kukicha tunalalamika ili au lile tunapopata watu wa kutuletea majawabu ya matatizo yetu pia tunalalamika ni kipi hasa tunataka jamani?!

Hatuwezi kuwakamata mafisadi wote siku moja, huu ni mwanzo na ni hatua nzuri watu wa Mara hawajui blaa blaa walipo ni wachapakazi tuu. Angalia usije ukawa ndugu wa kigogo huyo aliyefungiwa akaunti.

Nyoka ni mtoto wa nyoka; ukimuua, yule aliyemzaa ataza mwingine. Dawa ni kuua yule nyoka anayewazaa nyoka hao wengine.

Ubinafsi haujali umri,cheo,elimu,mamlaka..,haujali hasara,maisha ya wengine,..Watanzania ni wakati wa kubadilika.Kila mtu anahitaji maisha bora.Tuwe mawakili wazuri wa mali za umma kwa manufaa ya umma.Utajiri upatikanao kwa hila hautuongezei maisha marefu,bali AIBU ya sasa na ya Baadaye.Mungu Ibariki Tanzania.Mungu wabariki Viongozi wetu, watangulize TAIFA kwanza,Utumishi kwanza.

Kwa kweli TANESCO wametuchosa Watanzania! Limekuwa shirika sugu na chafu kwa muda mrefu. Swala kubwa kwa TANESCO ni wafanyakazi duni wasiojua wajibu wao na kuendekeza rushwa. Mfano mzuri ni viituo vile vilivyoweka kama vile cha TAZARA, Kinyerezi, n.k. Mambo yanayofanyika kwenye vituo hivyo ni uozo mtupu! ambao uongozi wa juu usipofuatilia shirika litaendelea kuangamia huku wachache wakijinufaisha na jasho la umma.

Watanzania sasa tumechoka kusikia wanasiasa wanayumbisha nchi mpaka  inafikia Bunge au Wabunge kutaka kuhalalisha Ufisadi, kweli inauma sana . Tunawasubiri na kamati zao waje sie wananchi sio wajinga tunaona na kusikia .
Mtu mwema na muadilifu anapigwa vita eti kwa maslahi ya wachache sasa tunasubiri hiyo kamati ije.
Tutapita nchi nzima kuwatangaza wote hao kwa majina bila kujali chama , maana nawapinzani nao wamo katika ufisadi  huo wanachi wawaadhibu maana tulidhani wapinzani ni waadilifu kumbe mafisadi watupu.
Tuwaunge mkono viongozi wanaotetea wananchi

Kama kweli tunataka kuwajuwa  Viongozi wetu basi tukubali kama wote ni wezi,majangili,majambazi,waasherati na wahuni kupindukia.hizi ndio sifa zao na wako madarakani kwa kuogopana na kufichiana siri zao.
Kila mmoja ana scandal kumshinda mwenzake ,nani atamkamata mwenziwe ?. Watanzania wacheni kupepea mwiku  ushapowa huo kuleeenni tuuuuuuuuuuu

Toa maoni yako

ShareThis Copy and Paste